Ticker

6/recent/ticker-posts

Sita washambuliwa kwa tindikali

Watu sita wamejeruhiwa vibaya kwa kushambuliwa na tindikali katika jiji la London nchini Uingereza usiku wa kuamkia leo.

Jeshi la polisi jijini humo limeeleza kuwa msamalia mwema aliwapigia simu kuhusu tukio hilo majira ya saa mbili usiku katika eneo la Stratford Center mkabala na Westfield.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, watu waliojeruhiwa walikuwa katika makundi tofauti hali inayozua wasiwasi kuwa mshambuliaji au washambuliaji walilenga watu bila mpangilio.
Aidha, Jeshi hilo limesema linamshikilia mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 15 kwa tuhuma za kuhusika na shambulio hilo.

Post a Comment

0 Comments