Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
WINGA wa kimataifa wa Tanzania,
Simon Happugod Msuva amesema
kwamba kiungo Salum Abdul Telela
ni kati ya wachezaji waungwana
aliokutana nao Yanga SC na hawezi
kuwasahau kwa wema wao daima.
Msuva alikwenda kumtembelea
Telela mwishoni mwa wiki kabla
ya kurejea Morocco kufuatia kuja
nchini kuichezea timu ya taifa mechi
ya kirafiki dhidi ya Malawi Jumamosi.
Na mfungaji huyo wa bao la kusawazisha
la Tanzania katika sare ya 1-1 Uwanja
wa Uhuru mjini Dar es Salaam
akaenda kumtembelea mchezaji
mwenzake wa zamani wa Yanga
baada ya mchezo huo.
WINGA wa kimataifa wa Tanzania,
Simon Happugod Msuva amesema
kwamba kiungo Salum Abdul Telela
ni kati ya wachezaji waungwana
aliokutana nao Yanga SC na hawezi
kuwasahau kwa wema wao daima.
Msuva alikwenda kumtembelea
Telela mwishoni mwa wiki kabla
ya kurejea Morocco kufuatia kuja
nchini kuichezea timu ya taifa mechi
ya kirafiki dhidi ya Malawi Jumamosi.
Na mfungaji huyo wa bao la kusawazisha
la Tanzania katika sare ya 1-1 Uwanja
wa Uhuru mjini Dar es Salaam
akaenda kumtembelea mchezaji
mwenzake wa zamani wa Yanga
baada ya mchezo huo.
“Nilikwenda kumtembelea Telala, 
kwa sababu ni rafiki yangu sana
na tumetoka mbali, tuna historia,
alinipokea vizuri Yanga na akaishi
na mimi vizuri sana. Hata alipoondoka
niliumia sana,”alisema Msuva akizungumza
na Bin Zubeiry Sports – Online
jana kwa simu kutoka Morocco.
Msuva amesema kwamba Telela
ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa
sana na ambaye anaweza kucheza timu
yoyote nchi yoyote. “Mwenyewe
ameamua kurudi masomoni, mambo
ya soka hayapi kipaumbele tena,
”amesema ambaye pia alitembelea
timu yake ya zamani, Yanga mazoezini.
kwa sababu ni rafiki yangu sana
na tumetoka mbali, tuna historia,
alinipokea vizuri Yanga na akaishi
na mimi vizuri sana. Hata alipoondoka
niliumia sana,”alisema Msuva akizungumza
na Bin Zubeiry Sports – Online
jana kwa simu kutoka Morocco.
Msuva amesema kwamba Telela
ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa
sana na ambaye anaweza kucheza timu
yoyote nchi yoyote. “Mwenyewe
ameamua kurudi masomoni, mambo
ya soka hayapi kipaumbele tena,
”amesema ambaye pia alitembelea
timu yake ya zamani, Yanga mazoezini.
0 Comments