
Mkazi wa Dar es Salaam,
Robert Massawe (51) ambaye
polisi wanadai ni mtuhumiwa
hatari wa uporaji na mauaji
ameuawa kwa kupigwa risasi
na watu wanaodaiwa kuwa ni
wenzake.
Kabla ya kuuawa katika majibizano
Kabla ya kuuawa katika majibizano
ya risasi, mtuhumiwa huyo anadaiwa
kukamatwa na bunduki aina ya SMG
ikiwa na risasi 24, simu 19
zilizoporwa maeneo mbalimbali
na laini za simu 58. Taarifa
iliyotolewa jana na kamanda
wa polisi mkoani Kilimanjaro,
Hamisi Issah ilisema mtuhumiwa
huyo aliuawa juzi saa tisa alfajiri
wilayani Rombo na watu
wanaodaiwa kuwa watuhumiwa
wenzake.Kwa mujibu wa taarifa
hiyo, mtuhumiwa huyo pamoja
na mkewe walikamatwa
jijini Dar es Salaam na baada
ya kuhojiwa na polisi anadaiwa
kueleza matukio mbalimbali
ya ujambazi aliyoshiriki.
Kamanda Issah alisema baada
ya kukamatwa jijini humo na
kuwaeleza polisi ushiriki wake
katika matukio mbalimbali ya
ujambazi alikubali kuwaonyesha
mahala alipoficha bunduki hiyo.
Polisi waliandamana naye
chini ya ulinzi mkali hadi
Moshi kwenye dampo lililopo
karibu na kiwanda cha ngozi
ambapo bunduki ilipatikana
ikiwa imefukiwa ardhini
ikiwa na risasi 24. “Muda
wote alitoa ushirikiano
mkubwa kwa polisi na
alivyokuwa akisimulia
matukio aliyoyafanya mwili
unaweza kusisimka.
Simu tatu kati ya 19
tumegundua ziliporwa
hapa Moshi,” alisema.
Katika mahojiano hayo
Katika mahojiano hayo
inadaiwa mtuhumiwa
huyo aliwaeleza polisi juu ya
mpango uliokuwapo wa
kufanya tukio la ujambazi
katika kijiji cha Chilio, kata
ya Holili wilayani Rombo juzi
alifajiri.“Akiwa chini ya
ulinzi wa askari kanzu
alikubali kuwapeleka
polisi katika eneo hilo,
sasa walipofika alipowaona
wenzake alipiga kelele ya
kuwajulisha wenzake kuwa
polisi walikuwapo eneo hilo,”
alisema.
0 Comments