Zlatan Ibrahimovic na Paul 
Pogba wataorodheshwa katika 
kikosi cha Manchester United
 katika mechi ya Jumamosi ya
 ligi ya Uingereza dhidi ya 
Newcastle katika uwanja wa
 Old Trafford.
Mshambuliaji Ibrahimovic , 36, 
bado hajashirikishwa katika 
mechi yoyote msimu huu baada
 ya kupata jeraha la goti mnamo
 mwezi Aprili.
Kiungo wa kati Paul Pogba , 
24, hajaichezea timu yake tangu 
alipopata jeraha la nyuma ya goti 
dhidi ya klabu ya Basel mnamo 
mwezi Septemba.
Beki Marcos Rojo pia anapatikana
 na mkufunzi Jose Mourinho 
alisema kuwa wote wataorodheshwa.
''Paul unaweza kuona. Unaweza 
kugundua kwamba kulikuwa 
na Manchester United msimu
 huu kabla na hata baada ya
 jeraha lake'', aliongezea Mourinho.
''Ana uwezo ambao hubadilisha
 vile tutakavyocheza mechi zetu''.
Mshambuliaji wa zamani wa 
Sweden Ibrahimovic ameichezea 
klabu hiyo mechi 46 na kufunga 
magoli 28 msimu uliopita.
Aliachiliwa na klabu hiyo mnamo 
mwezi Juni baada ya msimu 
wake kumalizwa na jereha la 
nyuma ya goti lakini akapewa 
mkataba mwengine mpya wa 
mwaka mmoja mnamo mwezi Agosti.
''Msimu uliopita tulimchezesha 
Zlatan kila dakika'', aliongezea 
Mourinho.
''Tulijifunza kucheza bila yeye.Lakini 
tunamkaribisha ni mchezaji mzuri sana''.