![Rais Magufuli Kuongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYPPZGjvih39XGkacNN736BZk7RNtlZOdHEwXwWb-eVqZ27SsbY2kZNQj53eiw-ll5s-uDmdCxHQYK1FY14SYBpM6RQHzdP7LrkAPEj7nwyWeua9DeA58l8hfBtVmH-F3AhaY3gpIFrFM/s400/CCM-3.jpg)
Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi
(CCM) inakutana jijini Dar es Salaam
chini ya Mwenyekiti Rais John Magufuli.
Kikao cha Kamati Kuu kinachofanyika
Kikao cha Kamati Kuu kinachofanyika
leo Jumatatu Novemba 20,2017
kitafuatiwa na kingine cha
Halmashauri Kuu ya Taifa kesho
Jumanne Novemba 21,2017.
Taarifa iliyotolewa awali na Katibu
Taarifa iliyotolewa awali na Katibu
wa Itikadi na Uenezi ya CCM,
Humphrey Polepole imesema vikao
hivyo pamoja na mambo mengine
vitakuwa na ajenda ya kupokea
tathmini ya uchaguzi mdogo wa
udiwani katika kata 43 ambao kampeni
zake zinaendelea.
“Ajenda nyingine ya vikao hivi vya
“Ajenda nyingine ya vikao hivi vya
uongozi vya kitaifa itakuwa kupokea,
kuchuja, kutoa mapendekezo na
kufanya uteuzi wa mwisho katika
ngazi ya mikoa na taifa katika chama
na jumuiya zake kwa maana ya umoja
wa vijana, wanawake na wazazi,”
ilisema taarifa ya Polepole.
CCM sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi
CCM sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi
wa ndani kuanzia ngazi ya shina mpaka taifa
(CCM) Ndugu Abdulrahman Kinana
akithibitisha kutimia kwa akidi kabla
ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu
ya CCM jijini Dar es salaam
kinachoongozwa na Mwenyekiti wa
chama hicho Rais Dkt. John Pombe
Magufuli leo Jumatatu Novemba 20, 2017
0 Comments