FAMILIA ya aliyekuwa Kocha
Msaidizi wa Timu ya Rayon Sports
ya Rwanda, Hamad Ndikumana
‘Katauti’ (39), imezuia staa wa
filamu Bongo, Irene Uwoya ambaye
alikuwa mke wa jamaa huyo asifanyiwe
fujo baada ya kutinga nchini
Rwanda jioni ya Ijumaa iliyopita.
Hatua hiyo ilikuja baada ya
Ndikumana kupoteza maisha huku
Uwoya akishushiwa tuhuma za hapa
na pale na kwamba huenda alichangia
kifo hicho.
Kwa mujibu wa chanzo chetu
Kwa mujibu wa chanzo chetu
kilichoambatana na Uwoya, familia
ya Ndikumana ilichukua uamuzi huo
baada ya watu mbalimbali nchini humo
kuwa na hasira na Uwoya. Kutokana
na kifo cha Ndikumana, Uwoya
alilazimika kwenda Rwanda kuhani
msiba akiwa na mwanaye aliyezaa na
jamaa huyo, Krish, mama na baba
yake na mabaunsa wa kumpa ulinzi.
Chanzo hicho kilieleza kwamba, watu
Chanzo hicho kilieleza kwamba, watu
mbalimbali nchini humo walikuwa na
hasira juu ya Uwoya kwamba ndiye
aliyesababisha kifo cha Ndikumana
kwani alikuwa na msongo wa mawazo
akimfikiria yeye kwa kuwa alimpenda
na kutaka wairudishe ndoa yao,
lakini mwanamama huyo akawa
anang’ang’ania apewe talaka
ambayo hadi Ndikumana anafariki
dunia alikuwa hajaitoa.
Staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya.
“Mashabiki wa Ndikumana walitaka
Staa wa filamu Bongo, Irene Uwoya.
“Mashabiki wa Ndikumana walitaka
kumfanyia fujo Uwoya kwa kuwa
wanadai ndiye chanzo cha kifo cha
mpendwa wao, lakini familia
iliwazuia wasifanye hivyo kwa
kuwa walishamsamehe Uwoya
ndipo hali ya amani ikawepo,”
kilisema chanzo hicho. Kiliendelea
kueleza kuwa, Uwoya aliwasili
nchini Rwanda Ijumaa iliyopita
kwenda kuona kaburi la mumewe
ambaye alizikwa Jumatano iliyopita
ambapo alipokelewa vizuri na
mama wa Ndikumana pamoja na
familia kwa jumla.
“Zile tofauti waliziweka pembeni
“Zile tofauti waliziweka pembeni
na mama Ndikumana akamwambia
wamemsamehe hivyo ikawa ni
kuomboleza upya kwani Uwoya
na mama’ke alikuwa akilia sana
hadi kushindwa kutembea
,” kilisema chanzo hicho. Hata
hivyo, alisaidiwa kwa kushikwa
mkono na wenyeji kwani mama
huyo alikuwa akimpenda sana
mkwewe Ndikumana kama mtoto wake.
Baada ya chanzo kutiririka, Ijumaa
Baada ya chanzo kutiririka, Ijumaa
Wikienda lilimtafuta Uwoya ambaye
alikiri kupokelewa vizuri na familia
pamoja na mama Ndiku ambaye
alipomuona tu alimkumbatia huku
akilia kwa uchungu akimuita ‘mwanangu’.
Naye msanii wa filamu, Michael
Sangu ‘Mike’ ambaye ni mmoja
wa watu waliosafiri alikiri kuwa
walipokelewa vizuri na hakuna
tofauti yoyote iliyojitokeza.
“Uwoya, baba, mama na Krish
“Uwoya, baba, mama na Krish
walitangulia na ndege na
walipokelewa vizuri kabisa na
hakuna mtu aliyewafanyia fujo
wala nini, familia imewapokea
kwa ukarimu na sisi ambao
tulifika baadaye maana tulisafiri
kwa basi tulipokelewa vizuri
sana,” alisema Mike Sangu.
Chanzo: Global Publishers
Chanzo: Global Publishers
0 Comments